Tuesday, June 26, 2012

Mgomo wa Madaktari kuanza kesho

 MADAKTARI wametangaza kuanza kwa mgomo kesho mpaka hapo serikali itakapokuwa tayari kutekeleza madai yao.

Pia wamesema kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amelidanganya Bunge kwa kusema kuwa madai ya madaktari tayari yameshashughulikiwa wakati siyo kweli.

Hayo yalisemwa jana na kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dkt. Steven Ulimboka, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam

Amesema kuwa, hadi sasa hakuna makubaliano yoyote yaliyofanyika kuhusiana na madai ya madaktari yaliyokuwa yakilalalamikiwa nyuma.

Amesema Awali madaktari hao walikubali kurudi kazini kwa kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliwataka kurejea kazini kwa ahadi ya kushughulikia madai yao

Amesema hayo yamekuja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kulidanganya Bunge kwa kusema kuwa madai ya madaktari tayari yameshashughulikiwa wakati siyo kweli.

“Waziri Mkuu, amelidanganya Bunge wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo, kwa kusema kuwa madai kumi waliyowasilisha, matano yameafikiwa na kila upande” jambo ambalo si kweli.

Pinda alilieleza Bunge kuwa serikali iliunda kamati maalumu ya kushughulikia madai yao kumi, matano yameafikiwa na kila upande.

“Baada ya hatua zote hizo kwa mujibu wa sheria ni lazima makubaliano yao yasajiliwe na Tume ya Usuluhishi (CMA), na kwamba hilo limefanyika ambapo tume ya serikali na upande wa madaktari wamemaliza kazi yake.

“Kati ya madai waliyoyataka serikali imeyatekeleza ni pamoja na kuondolewa kwa mawaziri wa wizara hiyo, kuongezwa posho ya kuitwa kazini, kufanya uchunguzi wa maiti na nyinginezo,

“Mambo matano waliyoafikiana ni serikali kukubali kuongeza posho ya kuitwa kazini kutoka sh 10,000 hadi sh 15,000 kwa madaktari walio kwenye mafunzo kazini na sh 20,000 kwa madaktari na sh 25,000 kwa madaktari bingwa.

“Pia serikali iliongeza posho ya uchunguzi wa maiti kutoka sh 10,000 hadi 100,000 kwa madaktari na sh 50,000 kwa wasaidizi, alisema Waziri Mkuu Pinda.

Ikiwemo na serikali kukubali kuwapa kadi ya Bima ya Afya ya rangi ya kijani ambayo ina hadhi ya huduma za daraja la kwanza kwa madaktari, pia kutoa chanjo ya ugonjwa wa ini ambapo fedha za chanjo hiyo zimo kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2012/2013.

Hata hivyo, maelezo hayo yalipingwa vikali na Chama cha Madaktari (MAT) na kupeleka kutangaza mgomo huo jana
Akiongea wakati akitangaza mgomo huo kwa niaba ya madaktari wenzake, Ulimboka alisema kuwa katika madai yote ya madaktari hakuna dai hata moja ambalo limetekelezwa kama alivyoeleza Waziri huyo

No comments:

Post a Comment