Saturday, December 1, 2012

Mjue Raisi Masikini Kuliko Wote Duniani



 
Raisi Jose Mujica wa Uruguay
Hebu fikiria viongozi wa Tanzania (raisi, mawaziri na wabunge) wangekuwa wazalendo kama Jose Mujica, natumai kwa utajiri uliopo Tanzania basi wananchi wangekuwa na maisha mazuri na Tanzania ingekuwa mbali sana.
Raisi Jose Mujica wa Uruguay (Amerika kusini) mwenye umri wa miaka 77 tokea alipochaguliwa kuwa raisi mwaka 2009 bado anaishi kwenye nyumba yake. Alipoulizwa na watangazaji wa BBC waliomtembelea nyumbani kwake ni kwanini hataki kuishi Ikulu, raisi Mujica alisema kuwa hahitaji kuishi kwenye jumba kubwa.
President Mujica's house
Hii ndio nyumba anayomiliki na kuishi raisi wa Uruguay na amekataa kujengewa nyumba nyingine mpya. Water supply ya nyumbani kwake ni kutoka kwenye kisima alichochimba mwenyewe na kuunganisha hadi ndani. Nyumba inalindwa na askari na kakataa kuwekewa fence kubwa kuzunguka shamba lake ili kuimalisha ulinzi wa nyumba.

President Mujica's VW Beetle
Gari analomiliki raisi ni Vokswagen Beatle yenye umri wa miaka 25 (toleo la mwaka 1987), pamoja na tractor analotumia kwa kilimo.

Raisi Mujica alishinda uchaguzi wa uraisi mwaka 2009. Asilimia 90, equivalent to $12,000 (£7,500) ya mshahara wake kwa mwezi hupeleka kwenye charity na kusaidia jamii masikini (hasa za mashambani) kwa shule, hospitals na huduma nyinginezo za jamii. Mawaziri wake walimwambia kuwa atumia pesa yake nyingi mno kusaidia watu, yeye anajibu kuwa hiyo asilimia 10 (£485) inayosalia kwa mwezi inamtosha kuishi maisha mazuri, hahitaji pesa nyingi na wala mavazi mengi. Salio hilo la mshahara wake ni sawa karibu na mshahara wa watu wa kawaida nchini Uruguay.

Charismatic Uruguayan president Jose Mujica has refused to adapt his lifestyle to match the trappings of wealth that come with being the country's most powerful figure
Raisi Mujica na tractor yake kwenye shughuli za kilimo.

Raisi Mujica anamiliki nyumba mbili za kawaida na moja iko shambani anakoishi, tractor ajili ya shamba na gari aina ya Volkswagen Beatle kwa matumizi yake na mkewe. Alipoulizwa na BBC team nyumbani kwake kuwa anajisikiaje kuitwa na wananchi wake kuwa yeye ni raisi masikini duniani, yeye anajibu kuwa yeye sio masikini na wala hajisikii kuwa masikini. Asema kila mtu ana uhuru wa kuishi maisha anayotaka, anaishi vyema kwa hivi alivyo navyo. Na ameishi maisha haya maishani mwake mote. Aongeza kuwa masikini ni wale wanao fanya kazi nyingi kujaribu kuishi maisha makubwa ya kifahari na wakipata hawaridhiki wanataka tena na tena na tena, utajiri wa mali hauleti furaha, utajiri ni kuridhika na vile ulivyo navyo.
Raisi Mujica anapokuwa likizo hutumia muda wake mwingi na mkewe kwenye shughuli za kilimo hasa cha maua. Na pia hujumuika na wana kijiji eneo ambalo anaishi kwa miaka mingi katika shughuli za kilimo na maendeleo iwe kutengeza mitaro ya maji au kujumuika na wazee.

Mr Mujica gives 90 per cent of his monthly salary, the equivalent of £7,500 away to charity, leaving him with just £485 a month to live off
Raisi Mujica akibeba dumu la maji shambani mwake


Mr Mijuca's proudest and most valuable possessions are his tired-looking Volkswagen Beetle and of course his three-legged dog Manuela
Raisi Mujica akiwa na mbwa wake mwenye miguu mitatu anayeitwa Manuella

No comments:

Post a Comment