Saturday, July 20, 2013

THE WORST VALENTINE’S DAY...SEHEMU YA PILI




SEHEMU YA PILI
susatule@gmail.com

Alinitazama machoni na ndipo nilipoona macho yake yakiwa mekundi na miale ya moto ilioneka na kwenye macho yake,,meno miwili marefu yalichomoza mdomoni kwake na ile hali ilizidi kunitisha na nilitamani nife ili nisione yaliyokuwa yanatokea,,alinisogelea na kunishika na kisha akanisemesha kwa lugha ya kiarabu lakini sikuelewa aliirudia tena ile lugha na wakati huu akinisogelea kwa karibu,,nilitetemeka sana na kwa muda mfupi nilikuwa tayari nimekonda lakini sikuweza kusogea wala kupiga kelele, wakati huo wale wengine walikuwa bado wamejifunika usoni na vitambaa vyeusi na walikuwa wameinama kama wanasujudu,,,haya yote yalikuwa maajabu kwangu,,,taratibu nilianza kuona ule ukuta wa nyumba ukirudi kama mwanzo na umeme ukarudi nilitazama pale sebuleni palikuwa pakubwa na idadi ya watu waliokuwa pale walikuwa ni zaidi ya hamsini na kulikuwa na boksi kubwa nyuma yao kama vile la friji,,hapo Jamshid aliendelea kunitazama na kuniongelesha kwa ile lugha ya kiarabu hata ivyo sikujibu kwakuwa sikuielewa na hapo alibadili lugha na kuanza kuongea Kiswahili;
“Asalam aleyku”alinisalim mara hii kwa salam ambayo nayo sikuweza kuijibu,,
“Jina langu naitwa jini Shamsu, naishi katika kilindi cha maji ndani ya bahani ya hindi nyumbani kwetu ni Nungwi, mbele yako kuna majini tofauti zaidi ya 50 ila niwatambulishe kwa majina wakuu wangu,,ATHA huyu ni mkuu wangu, ndiye mungu wa kiarabu wa kuabudu sanamu,,yupo TARAKADHURU jini lililompa baba yako mali kwa masharti akakiuka,,yupo jini AL-RAHAB aliyekukatia umeme wakati tunakuja,,yupo jini ABADI ambaye ndio yeye na kundi lake waliohusika kuvamia nyumba yenu na kumbaka mama yako mpaka kufa,,yupo jini FARK na majani mengine”. Ilikuwa sauti ya Jamshid ikiongea hayo yote ambayo kwangu mimi sikuyaelewa na hapo akili yangu ilihama na kurudi miaka mingi nyuma wakati wale majambazi wameivamia nyumba yetu,,,ilikuwa ni majira ya saa nane usiku ambapo nilikia sauti ya baba na mama wakipiga kelele nikashtuka na muda mfupi mbele nikatoka mpaka kwenye korido na ndipo nilipokamatwa na kupelekwa moja kwamoja mpaka pale walipowekwa wazazi wangu na mimi nikafungwa pamoja nao,,mama yangu alichukuliwa na kuvuliwa nguo mbele yangu na baba na kisha walianza kumuingilia mmoja baada ya mwingine,,,alilia kwa uchungu sana lakini hakuna ambalo tungeweza kufanya nakumbuka yale majambazi yalimgeukia baba na kuanza kumsemesha kwa lugha ambayo hata ivyo sikuielewa na baba aliwajibu huku akionekana kuzidi kuomba msamaha,,kwakuwa akili yangu ilikuwa ndogo sikuwaza ile ni lugha gani na kwanini mambo yote yalitokea kwa haraka,,,nakumbuka kesho yake asubuhi mama alifariki lakini usiku ule baada ya wale majambazi kuondoka nilimsihi baba tumpeleke hospitali lakini alikataa na badala yake alimpigia simu mtu nisiyemfahamu na kuongea nae kwa lugha ileile ile ambayo wale watu waliongea nae na sasa ndo napata akili kuwa lugha ile ilikuwa ni kiarab,,siku moja baada ya mazishi ya mama nakumbuka vizuri kuwa baba aliniita na kuni na kunikalisha chini na maongezi yetu yalianza kwa yeye kunipa mlolongo mrefu wa mambo ambayo hata hivyo sikuelewa maana hakuwa wazi;
“Binti yangu mama yako amefariki na hatuna la kufanya juu ya hilo,,wewe una umri mdogo lakini kuanzia hivi sasa unatakiwa ujifunze kujitegemea na kuongoza biashara zangu na miradi mingine” hiyo ilikuwa sauti ya baba yangu ikinipa taarifa na hapo ilikuwa ni siku moja kabla ya kifo chake
“baba tupo wote mimi sidhani kama nitaweza kufanya hayo”nilimuambia kwa sauti ya upole lakini nilishangaa baba alivyoamka na sauti ya ukali
“utaweza na ni lazima uweze,,usiseme tupo wote,,” hiyo ilikuwa sauti ya baba yangu ikinipa taarifa na hapo ilikuwa ni siku moja kabla ya kifo chake
“baba tupo wote mimi sidhani kama nitaweza kufanya hayo”nilimuambia kwa sauti ya upole lakini nilishangaa baba alivyoamka na sauti ya ukali
“utaweza na ni lazima uweze,,usiseme tupo wote,,you are only you,,am dead already (uko peke yako, mimi nimeshakufa tayari)”..Nilishangazwa na taarifa hii lakini zaidi sikutilia maanani maneno ya baba kwakuwa nilijua ni msongo wa mawazo kwa kifo cha mke wake, lakini alinyanyuka pale na kusimama pembeni akachukua simu yake ya mkononi na kuanza kupiga simu na hapo nilimsikia akiongea na mtu kwa lugha ya kifaransa;
“la cargaison est arriv
ѐѐ?” (Mzigo uliwasili?) Ilikuwa sauti kavu ya mzee ikiuliza na baada ya upande wa pili kujibu nilisikia tena akimsemesha kuashirika kuwa tayari walishakubaliana.
“Venez chez moi maintenant” (Njoo nyumbani kwangu sasa hivi),,baada ya hapo baba alibonyeza teza vitufe vya simu yake na akaiweka tena sikioni na sasa alikuwa akiongea na Rorbahcho rafiki yake wakijerumani aliyekuwa akiishi Tanzania ambaye ndiye niliyekuwa nikimchukulia kama baba yangu mdogo kwakuwa sikuwahi kumuona ndugu ya baba yangu,,,waliongea kwa sauti ya chini lakini niliweza kumsikia baba akimueleza jambo na kwakuwa nilielewa japo ni kidogo nilimuelewa;
“Ich konnte jeden Tag ab heute sterben” (ninaweza kufa siku yoyote kuanzia leo) hili lilikuwa kati ya maneno machache sana ambayo niliyasikia katika yale maongezi ambayo baba aliongea na Mzee Rorbahcho lilinishtua na kuniumiza ila sikuelewa chochote kilichokuwa kikiendelea pale niliendelea kumsikiliza akiongea na nilibahatika kusikia maneno mengine na kiasi cha pesa kilichonishtua;
“make 200,000/= pfund auf meiner tochter-konto übertragen”(hamisha paundi 200,000 taslim kwenda kwenye akaunti ya binti yangu),,fedha hii ilikuwa ni sawa na shilingi za kitanzania milioni mia tano,,nilitaka kumuuliza baba nini kilikuwa kinaendelea lakini sikupata mda wa kufanya ivyo kwani baada ya yeye kumaliza kuongea na simu hiyo alimpigia simu Samah Jiraz ambaye ni binti mwenye asili ya kiarab na mda si mrefu niliona akiingia na gari yake nyeusi aina ya Cadillac,,Samah alikuwa ni mwanasheria wa familia yetu na baada ya yeye kufika kwa haraka niliitwa ndani na makabidhiano ya mali yalianza,,mambo yalikwenda haraka sana na sikuweza kuuliza chochote zaidi ya kuweka sahihi kwenye lundo la makaratasi yaliyokuwa pale mezani,,na baada ya muda mfupi tulimaliza na Samah aliambiwa anipeleke kwenye kila sehemu ambayo tumeweka sahihi makatasi yake,,,niliingia kwenye gari ya Samah na muda mfupi mbeleni tuliingia kiwanda cha Maji ya kunywa cha MORIS FOOD INDUSTRIES na hapo alikusanya wafanyakazi wote na kunitangaza kama mmiliki wa kiwanda hicho,,,hakuna aliyehoji na sikuwa naelewa nini kinaendelea bado,,,niliingia kwenye gari na moja kwa moja nilipelekwa maeneo mengine mengi na mida ya saa saba tuliingia kwenye nyumba kubwa ambapo ndani nilikutana na mwanamke mrembo aliyevaa baibui ya rangi ya dhahabu na Samah alinitambulisha kuwa yule aliitwa Maysa ndiye aliyemsaidia baba yangu kupata uraia wa Tanzania kipindi alipoingia nchini akitokea Rwanda enzi izo akiwa kijana,,alinifahamisha kuwa Maysa alikuwa ni Msaidizi wa balozi wa Oman nchini Tanzania lakini hata hivyo sikuelewa kwanini tuko pale,,,waliniingiza ndania na mara hiyo Maysa aliniambia nisiogope chochote na akaja mbele yangu na chupa ya juice na kuniwekea nilipoinywa nilitapika lakini alichoniambia ni kuwa sasa naweza kujitegemea yote yalitokea haraka na hakuna muda wa kuuliza swali nilikuwa kama nimepigwa na butwaa lakini baada ya kunywa ile juice nilipata nguvu za ghafla na woga uliniishia.
*****
“Faith” nilishtuka toka kwenye dimbwi la mawazo lililonifanya nisahau kilichokua mbele yangu.
“Abee” niliitika kwa sauti ya mshtuko iliyojaa woga na kilio,,Jamshid alinyanya mikono yake kama aliyekuwa akiagiza kitu na hapo wale watu wote walikaa pande mbili na katikati yao kukatokea sufuria kubwa lenye maji ya moto yanayochemka.
“Leo ni siku ya wapendanayo na ni siku ya kutimiza maagano,,ni siku ya malipizi ni siku ya adhabu kwa wote waliosaliti ufalme wa majani,,leo ni siku ya sherehe na leo ni siku ya kunywa damu,,leo ni siku ya kufunuliwa kwako na siku ya kujua ukweli unaouma” aliongea Jamshid na hapo aligeuka na kuongea na wale waliokuwa wameketi pale ambapo ukuta ulichanika na wao kuingia,,,aliwasemesha kwa lugha ya kidachi ambayo na mimi ghafla nilijikuta nikiifahamu;
“Brengen dat verrader hier” (mleteni yule msaliti hapa) hapo waliondoka wale jamaa kupitia ile kona ya ukuta na hapo walirudi na mtu kwenye kiti chenye matairi kupitia pale kwenye ule ukuta na alikuwa amefunikwa,,baada ya kumfikisha pale aliwanyanyua wengine na kuwaambia tena kwa lugha ile ile ila muda huu alisema kamleteni yule Malaya,,,baada ya hawa kutoka aliingizwa mtu mwingine akiwa na hali kama ile ya yule wa kwanza na hapo walifunuliwa vile vitambaa,sikuamini nilichokiona,,,alikuwa ni baba yangu na mama yangu wote wakiwa hai,,walikuwa wamekonda na walionekana wadhoofu kupita maelezo nililia kwa uchungu mkubwa na kutaka kuwafata lakini sikuweza kunyanyua mguu pale nilipokuwa,,nililia nikimuita mama na baba lakini haikusaidia mana wao pia machozi yaliwatoka na walionekana wakitaka kuongea lakini hali waliyokuwa nayo sauti haikuweza kutoka,,,hapo niliisikia tena sauti ya Jamshid ikiita na hapo wasichana wawili waembo waliamka na kutoa vitambaa vyao na mikononi walikuwa na mapanga mawili marefu yaliyokuwa yaking’aa kuonyesha kuwa yanilikuwa makali kama wembe,,,nilifuta machozi na kuwatazama usoni sikuamini kuwa wale walikuwa MAYSA NA SAMAH…

UNATAKA KUJUA KILICHOENDELEA????UMEUPENDA MKASA HUU NA HADITHI HII?? Hahaaa tuendelee kuwa pamoja

No comments:

Post a Comment