Afande Sele kulia, akiwa na mwanae Tunda
Wale wafuatiliaji wa muziki wa kizazi kipya 'Bongo Fleva' watakua
wanamfahamu vizuri Tunda ambaye ni mtoto wa mfalme wa Rhymes Tanzania,
Afande Sele. Tunda alipozaliwa takribani miaka 11 iliyopita, Afande Sele
alikua akimtaja sana katika nyimbo zake na alipokua akihojiwa.Hii
ilipelekea jina la Tunda kukaa vichwani mwa Watanzania hasa mashabiki wa
Afande Sele.Tunda huyu sasa ni binti wa miaka 11, na sasa yupo Kidato cha kwanza. Ni binti mwenye uwezo mzuri darasani. Alifanya mtihani wa Darasa la 7 kipindi alipokua darasa la 6 na kufanya vizuri. Hii ni kwa mujibu wa baba yake kama alivyoeleza hapo chini kupitia ukurasa wake wa facebook.
Hapa chini ni familia nzima ya Afande
Toka kushoto ni Tunda,Sanaa,Afande na Mkewe. Mambo ya nyota ya kijani umeyaona mdau?
No comments:
Post a Comment