Kutoka Morogoro
taarifa ni kwamba jeshi la polisi la mkoa huo limefanikiwa kukamata gari
ndogo aina ya Spacio likiwa na mwili wa marehemu ambapo zoezi hilo
limefanikiwa baada ya taarifa kutoka kwa wasamariawema.
Kamanda wa polisi mkoani mbeya
Faustine Shilogile amesema walipata taarifa za kuwepo kwa gari hilo
ambalo lilikuwa linatokea Mbeya kuelekea Dar.
Polisi wa mkoa wa Morogoro waliweka
mtego kwenye kituo cha Mikumi hatimaye na kufanikiwa kukamata gari hilo
likiwa na watu watatu,pipi saba za vitu vinavyosadikiwa kuwa ni dawa za
kulevya na mwili wa marehemu.
Mwili huo ulivyopelekwa hospitali na
kufanyiwa uchunguzi umekutwa na pipi nyingine kumi na saba tumboni na
inasemekana mtu huyo alifariki akiwa Mbeya.
Pipi hizi zimetolewa tumboni na
zinafanyiwa uchunguzi kujuikana ni kitu gani lakini shaka kubwa zinaweza
kuwa ni dawa za kulevya na haikuweza kuthibitishwa kwasababu bado
hazijapitia kwenye maabara kwa ajili ya kuzitambua ni dawa za aina gani.
Watu wote watatu ambapo wawili wanahusika na gari hilo na mmoja ni mfanyabiashara wa Kariakoo wanashikiliwa na polisi huko Morogoro.
No comments:
Post a Comment