Kwa nini mapenzi ni tata? Unaweza kujiuliza swali hilo. Ni kwa faida ya
kila mmoja kwa sababu yanatuhusu sote. Ni matamu lakini ndani yake
hutokea kuwa na ukakasi kama siyo maumivu.
Jiulize tena, kwa nini
mapenzi yanasumbua? Mapenzi ni maumivu ya kichwa na moyo. Watu wengi
waliomo ndani yake wanaweza kukupa ushuhuda wa mateso wanayoyapata
kwenye uhusiano wao. Je, baada ya kuteseka huwa wanajiapiza kutorudi
tena?
La hasha! Wanajaribu mara nyingi, hawakomi. Unaweza
kujiuliza ni kwa nini lakini ukweli ni kwamba pamoja na maumivu ambayo
mtu anaweza kuyapata kwenye mapenzi, bado yanabeba hisia kubwa katika
maisha ya kila binadamu.
Maisha bila mapenzi hayajakamilika.
Kutokana na hilo, uwanja upo wazi kwako kujiuliza ni kwa nini kitu
kitamu namna hiyo kikafanywa kuwa tata, jumlisha na maumivu ya hapa na
pale. Uvumilivu ukizingatiwa, huyeyusha utata unaojitokeza mara kwa
mara.
Muhimu zaidi ni kwamba mapenzi hayatoshelezi kwa
uwajibikaji wa nusu nusu. Yanahitaji nidhamu na utekelezaji wa moja kwa
moja kutoka moyoni. Yanayomhusu mwenzi wako ni vyema uyabebe kama yako,
hivyo ndivyo uhusiano unavyotaka.
Mapenzi yanahitaji akili,
utashi na fikra zako bila kusahau nguvu zote katika kuzalisha matunda ya
kila siku kwenye uhusiano ulionao. Utata unaoonekana ni ule unaotokana
na wenzi kutotimiza matarajio ya kila mmoja.
Imetokea kuamini
kuwa maneno ni mhimili wa kudumu kwa uhusiano na kukutana kimwili
husuluhisha migogoro ya muda mfupi. Wapenzi wanaponuniana, endapo
watakutana faragha, hasira zote hupotea. Hata hivyo, kwa bahati mbaya,
ni zaidi ya kutosheka kimwili na utamu wa maneno mazuri.
Kwa
mfano, ndoa nyingi zinakumbwa na matatizo ya watu kushindwa kuwa
wakweli. Mwanaume au mwanamke anaweza kusema ni kiasi gani mwenzi wake
anamuumiza. Lakini mwisho wa mazungumzo hawezi kukiri kasoro zake ambazo
pengine ndiyo chanzo cha kila kitu.
Utata zaidi katika mapenzi
ni kuwa, inapotokea watu wanajuana kwa undani mno, hasa baada ya kuishi
muda mrefu, ni hapo ndipo maneno hayawezi kufaa kitu, wala mchezo wa
faragha hautaleta maelewano kwa maana hakuna kitu kigeni.
Lingine
la utata katika mapenzi ni kwamba huwezi kuficha tabia yako muda wote.
Ukishazoeana na mwenzi wako hasa baada ya kuwa pamoja muda mrefu,
utaanza kujiachia. Ni kipindi ambacho mmoja anaweza kuhisi amesalitiwa
kwa sababu mwanzoni hakuona hivyo ‘vitabia vya kuudhi’, alifichwa.
MAPENZI NI KARATA TATU
Kuna
msemo kuwa mapenzi hayashindwi ila watu ndiyo hushindwa na mapenzi.
Tunarukia kwenye uhusiano bila kuwa na uhakika ni kiasi gani tunawapenda
wenzetu na ni kwa kiwango kipi tumejiandaa kubeba majukumu.
Mwisho
wake tunafeli. Tatizo ni kwamba tunaanzisha uhusiano mpya bila kutatua
kasoro zilizosababisha tukashindwa kwenye uhusiano na mtu wa kwanza.
Hapo nadhani unaweza kuona kwamba wakati mwingine mapenzi siyo tata ila
wenyewe tunayafanya kuwa magumu.
Tuna mambo mengi, ya kifamilia,
kikazi, imani, dini, kabila, tofauti za kimtazamo na matarajio ya kila
mmoja. Hatuko sawa. Tunapoingia kwenye uhusiano, fikra zetu zinakuwa
zimejaa. Ajabu ni kwamba tunapoingia kwenye uhusiano hatuyapi kipaumbele
katika kuyajadili na kukubaliana. Hisia za juu hutupeleka kama vipofu.
Uhusiano
wa kimapenzi wa watu wengi huanza pale ambapo mtu anajihisi yupo mpweke
na anahitaji kampani. Wakati mwingine inatokea kwa sababu mtu anakuwa
anakabiliwa na ‘presha’ ya kuwa na mwenzake kwa kigezo kwamba umri
umekwenda. Si kwamba amemuona mtu mwenye sifa anazohitaji.
Umri
ni kigezo kimoja lakini inawezekana ikawa mtu anataka kuwa na mwenzake
kwa sababu ya msukumo wa nafasi yake kwenye jamii au kimila. Pengine ni
dada sasa wadogo zake wameolewa yeye bado yupo tu. Au ni kaka, kwa hiyo
kama kiongozi wa familia anaona bora aoe mapema kabla ya wadogo zake.
Kama
umeingia kwenye uhusiano kwa sababu ya presha ya aina hiyo, utawezaje
kuwa na matunda sahihi? Kichocheo cha uhusiano wa kimapenzi kinapaswa
kuwa mapenzi. Mnapendana, kwa hiyo nyoyo zenu zinavutana kuingia kwenye
sayari maalum.
Usiwe na papara, angalia mahitaji ya moyo wako,
weka mbele matarajio yako. Fikra zako uziweke wazi. Unapotafuta mwenzi
hakikisha husumbuliwi na presha yoyote. Jambo ambalo unapaswa kuamini ni
kwamba aliye ndani ya mawazo yako utampata kama ukijipa nafasi.
Kuna mambo ya kufanyia kazi, uki yahitaji kujua niulize kupitia .....email yangu...........nasri.selemani@yahoo.com ....au .....susatule@gmail.com
pia unaweza kuandika swali lako kwa sms kisha tuma namba hii 0718 363624 utajibiwa bureeeeeeeeeeeeeeee.....
No comments:
Post a Comment