Friday, November 9, 2012

Temeke yakanusha kuwa na watu walionasiana wakingonoana


Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk Amani Malima (pichani) amekanusha uvumi wa wapenzi wawili kunasiana na kufikishwa katika hospitali yake .Akizungumza na waandishi wa habari alisema kwamba hakuna tukio kama hilo hospitalini hapo na alisikitika kuwa limesababisha wasitishe huduma kwa zaidi ya saa saba.
“Huduma haziendi kama kawaida, hatujui ni nani aliyevumisha habari hiyo, cha kusikitisha hata baadhi ya vyombo vya habari vimeripoti, kwamba tukio hilo lipo kama vile waliliona, huu ni uongo, iwe wafu au wazima, sijaona watu kama hao hapa,” alisema Dk Malima.
Mitandao ya kijamii ilidiriki hata kuweka picha ambazo nyingi zikionesha kama zimechezewa zikidai kuwa watu wapo hospitali ya Temeke.
Baadhi ya watu walidai kuwaona wawili hao waliong’ang’aniana walidai, walikumbwa na mkasa huo katika nyumba ya kulala wageni na mwanamke, ndiye sababu ya tukio hilo baada ya kutegewa na mumewe.
“Hilo tego ni la mwanamke, yaani ukimwona yule dada huwezi kuamini, mimi nimemwona maana ninafanyakazi huko hospitalini, ni aibu, wamefunikwa kwa shuka la gesti, suala hilo si la kutibiwa hospitalini ni mpaka mumewe aje ndio watengane,” alisema msichana mmoja.
Baadhi ya watu nje ya hospitali walisikika wakisema mmoja kati ya watu hao amekufa, wengine wakidai wote wawili wamekufa kwa shinikizo la damu, lakini walipohojiwa zaidi walishindwa kutoa uthibitisho wa maelezo yao.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, David Misime (aliyehamishiwa Dodoma), akizungumza kwa simu, alisema ni uvumi  usio na ukweli.

No comments:

Post a Comment