Sunday, July 28, 2013

SEHEMU YA NNE..THE WORST VALENTINE’S DAY



 
THE WORST VALENTINE’S DAY
SEHEMU YA NNE
susatule@gmail.com

ILIPOISHIA
,,,nilimtazama mama yangu aliyekuwa amekonda kupita kiasi na ndipo nilipopaza sauti;
“COOOMEEEE THE ANGEEELLLLS OFFFF LIIIGGHHT”(njooni malaika wa nuru),,,nilipaza sauti mara tatu na ngurumo kubwa za radi ziliitikisa ile nyumba moto mkubwa ukawaka na mvua kubwa ikaanza kushuka,,,Jamshid alinisogelea na lile panga kwa karibu na kuniuliza mimi ni nani na nina nguvu gani,,,na mimi nilimjibu kwa sauti kuu…
“Am a FREEMASON”

SONGA NAYO
“unasema nini” nilisikia sauti ya Jamshid ikiuliza kwa shauku ya kutaka kujua nilichokisema,,mda huo wale wengine wote waliyeyuka na sikujua walitokaje pale,nilipotazama pale ndani hata hivyo nilimwona Magret tu ambaye alikuwa bado pale chini.
“kama ulivyosikia”nilimjibu Jamshid na kukimbia pale alipokuwa Magret nikamnyanyua na ghafla nilishangaa kuona lile ziwa likiwa halijakatwa,,hapo bado ngurumo za radi na ule moto uliendelea kuwaka na ndipo niliponyoosha ishara ya vidole viwili na pale kila kitu kilitulia,,,sikumwona baba yangu wala mama yangu na pale ndani palikuwa shwari kabisa,,niligeuka tena na sasa nilimuona Jamshiod aliyekuwa amesimama huku akitetemeka na mda huu alikuwa katika hali ya kibinadamu..nilimsogelea na hapo nilipata ujasiri mkubwa wa kumpiga kofi shavuni;
“nakuchukia kuliko kitu chochote katika maisha yangu,,ondoka hapa”,,nilimwambia Jamshid na hapo nilishuhudia machozi yakimtoka na sauti yake ilisikika ikiniambia;
“sina hatia,,ipo siku utaujua ukweli Faith” aliniambia na muda huohuo sikumuoana tena,,nilikaa pale chini nikalia kwa uchungu sana na ndipo nilipomwona Magret akifungua macho taratibu,,nilimkimbilia pale chini na ndipo nilipogundua Magret hakufahamu lolote lililokuwa likiendelea;
“kwanini unalia dada Faith” ndilo swali la kwanza alilonihoji na nilijitahidi kumficha ukweli wa mambo ili kama ni kweli hatokumbuka basi katika maisha asikae akumbuke lile tukio lililotokea pale,,sikutamani kabisa mtu yoyote afahamu kilichotokea kwakuwa hata mimi nilitamani kuusahau ukweli niliouona,,,maswali mengi yalikijaza kichwa changu lakini kikubwa ni wapi wamepelekwa wazazi wangu na ni kwanini Jamshid alibaki nyuma,,mapenzi na Jamshid sikuyawaza tena na sasa nilihisi maisha yangu yameshaharibika kabisa siri zangu zimeshabainika na sasa kila mtu atajua kuwa najihusisha na kundi ambalo wengi wanaliogopa;
“dada Faith”,,ilikuwa sauti ya Magret ambaye alikuwa tayari ameshaamka pale chini na nilimuona akiwa amesimama dirishani,,hapo woga ukanijia tena upya.
“unasemaje”nilimuuliza kwa shauku maana alionekana na yeye alikuwa akitazama nje.
“kuna magari matatu yameingia kwetu meusi,njoo uyaone”nilinyanyuka pale nilipokuwa na moja kwa moja nilienda mpaka dirishani nakutazama nje, ndipo nilipogundua kuwa walikuwa ni wakuu wa kundi la freemason nchini Tanzania,,hofu ilinijaa na hapohapo nilisikia tumbo likikata,,nilimwambia Magret kuwa wale walikuwa wageni wangu na nilimuomba aende chumbani,,,na mimi nilitoka taratibu nikaingia chumbani nikavaa gauni langu refu na kisha nilitoka mpaka pale nje ambapo moja kwa moja nilikutana na mzee Vladimir ambaye ndiye mwenye cheo kikubwa kwa hapa Tanzania;
“vi salute nel nome di angeli della luce”(nakusalimu katika jina la malaika wa nuru) nilimsalimu kwa lugha ya kiitaliano kwakuwa ndiyo lugha niliyoambiwa kuitumia wakati nikisalimiana na mkubwa wangu,,,alininyanyua pale nilipopiga magoti na kuniangalia machoni kisha kunipa mkono kama tulivyozoea kupeana kwa ishara zetu,,,mawazo yangu yote hayakuwa pale, nilikuwa nikiwaza ni nini kitatokea kwakuwa kwa mara ya kwanza sasa toka nijiunge na kundi hili kwa ushawishi wa Mzee Rorbahcho aliyekuwa rafiki mkubwa wa baba yangu mpaka leo hii sijawahi kufatwa na viongozi wangu na leo ikiwa ndo nimetumia nguvu za wakuu wa nuru nimekuja kufatwa nyumbani,,hii kwangu ilikuwa ni hofu nyingine tena,,,akili yangu ilivurugika na sasa nilianza kujuta kila kilichotokea kwenye maisha yangu,,,saa yangu ya mkononi ilionyesha mda huo ulikuwa ni saa 5 na dakika 33,,ikimaanisha siku ya wapendanao ilikuwa bado haijaisha; nilipotazama vizuri alioongozana nao niligundua kuwa alikuwamo Mzee Rorbahcho nae alikuja na kunishika mkono..mpaka hapo ile hofu ikaondoka na ndipo niliposikia sauti ya yule kiongozi ikiniambia tena;
“Noi vi proteggera ma si fara presto il tuo sacrifice”(tutakulinda ila utatoa sadaka yako muda sio mrefu)..milishtushwa na neno sadaka lakini sikupata muda wa kuuliza kwani wale waliingia kwenye gari na kuondoka,,,bado akili yangu ahaikuwa sawa na sasa nilikaa pale chini tena nikilia,,,ila ghafla machozi yalinikauka baada ya kunyanyua uso wangu na kumuona Jamshid akiwa amesimama mbele yangu na kunipatia kitambaa ili nijifute machozi,,hasira zilinirudia tena na sasa nilitoka pale kwa kasi na kukimbilia ndani nikachukua bastola yangu na kutoka nje ambapo nilimkuta Jamshid akiwa amesimama palepale,,,niliikoki na kunyoosha kuelekea kwake na bila kuhoji mara mbili niliifyatua risasa mara tano mfululizo lakini hakuna hata moja iliyopenyeza mwili wake,,nilizidi kulia na kufyatua risasi ovyo huku nikimulekea yeye lakini niliishiwa tena na machozi nilipoona na yeye alikuwa akili,,katika hali isiyokuwa ya kawaida nilimtazama Jamshid na kumuonea huruma,,mara hii na mimi machozi yalinitoka si kwasababu nyingine ila nahisi ni kwasababu ya mapenzi niliyokuwa nayo kwa Jamshid,,nilijaribu kuidanganya nafsi yangu kuwa namchukia Jamshid lakini haikuwa hivyo katika uhalisia wake,,nilimpenda Jamshid kwa kila hali na kikuwa nilikuwa nikikumbuka aliponambia pale ndani kuwa alikuwa kama mimi lakini alikuwa alivyo kwa makosa ya wazazi wake..nilimsogelea pale alipokuwa amesimama na kwa sauti ya ukali iliyojaa mahaba nilimuuliza;
“unataka nini katika maisha yangu ewe jini usiye na haya”nilijitahidi kumkazia macho ili asione udhaifu wa kihisia ulioanza kutanda ndani ya uso wangu.
“Faith,,nililazimishwa kuwa hivi baada ya wazazi wangu kukiuka masharti ya jini lililompa utajiri baba yangu,,,baba yangu alikuwa ni mmiliki wa kisima kimoja cha mafuta huko uarabun,,kuna kipindi mafuta hayakuwa yanapatikana kabisa na ndipo alipoamua kwenda kutafuta namna ya kuhakikisha kisima chake kinatoa mafuta kama kawaida,,,alifanikiwa na kupewa kaya ya majini ili kufanya usimamizi wa shughuli zake kwa ahadi kuwa angenitoa sadaka lakini baadaye aliwakatalia na ndipo walipoanza kumuandama na kisha kumfilisi na mwishowe walikuja kumuua na nililazimishwa kunywa damu yake na toka pale niligeuka kuwa kama wao,,niliamia kisiwani nungwi chini kabisa ya bahari na kuishi huko nikinywa damu za watu waliopotelea baharini kwa muda wa miaka 7 na ndipo nilipopandishwa cheo na kuachiwa,,siipendi hali niliyopo na kwasasa nimefukuzwa na hawataniacha mzima mpaka niende na wewe,,,naamini unaweza ni saidia kwakuwa uwezo wako na wa watu wako ni mkubwa kuliko uwezo”,,,aliongea hayo Jamshid huku machozi yakimtoka,,,nilisikia uchungu kwa yale machache aliyoyaongea na hapo nilimfata na kumkumbatia,,,sikuamini kwa ulo msisimko niliousikia wakati namkumbatia Jamshid pale nje,,nilimkumbatia kwa takribani dakika tatu bila kumuachia na wala sikutamani kumuachia pia,,,alikuwa na mvuto wa aina yake kwa hakika ya moyo wangu huyu ndo alikuwa chaguo langu.
****
Nilimvuta mpaka ndani na ndipo niliponyanyua simu yangu ya mkononi nikampigia mzee Rorbahcho nikimuomba kuonana nae,,na yeye alinambia tukutane mda ule ule,,Lapodiz café iliyokuwa mita mia tano toka pale kwangu,,nilimuingiza Jamshid kwenye gari na kuondoa gari kwa kasi ya ajabu na ndani ya dakika tatu tulishafika,,nilishukla na kumueleza mzee Rorbahcho kila kitu na yeye aliniambia tunaweza kumsaidia Jamshid akarudi katika hali ya kawaida kwakuwa katika ulimwengu wa nuru mengi yanawezekana,,,hapo tulipanda gari yake na moja kwa moja tulielekea mpaka eneo letu la kukutania maarufu kama MASONIC LODGE,,na pale aliniacha nje na yeye na Jamshid waliingia ndani ambapo wakubwa wa kundi hili walikutana,,nilisubiri nje kwa masaa matatu na hapo sikupata usingizi hata kidogo,,baadaye walitoka na sasa Jamshid alionekana ni mzima kabisa,,nilielezwa kuwa watamlinda na hakuna nguvu inaweza kushindana nao.
****
WIKI MBILI MBELE
Haikuwa rahisi kumuonyesha Jamshid hisia zangu tena kwa siku zilizofuata japo aliishi nyumbani kwangu kwa takribani wiki mbili sasa mar azote alikuwa akijitahidi kuomba msamaha na kunieleza yale yaliyotokea hayakuwa katika mipango yake na sasa niliamua kumsamehe na sasa mapenzi yetu yalianza upya,,,Jamshid alifanikiwa kuuingia mwili wangu na kuweka historia ya kuwa mwanaume wa kwanza katika maisha yangu kushika mwili wangu na hata kuvua nguo yangu ya ndani,,nilisikia maumivu makali siku ile lakini raha niliyoipata iliziba maumivu yale niliyoyasikia,,na sasa maisha yalikuwa ni kati ya mimi na yeye na Magret ndani ya jumba letu kubwa lililojitenga na maeneo ya watu wengine,,,bado nilikuwa na hofu ya pengine labda hali ya hatari ingeweza kujitokeza tena lakini kwa maisha niliyoyaanza na Jamshid niliamini ningekuwa salama kabisa..nilimpenda Jamshid kuliko kitu kingine chochote,,upendo wangu kwa Jamshid ulikuwa sawa na nilivyompenda Magret japo kwa Magret ulizidi kiasi kwakuwa yeye alikuwa ni sehemu ya maisha yangu,,Jamshid na Magret kwasasa ndio walikuwa baba yangu na mama yangu, niliwapenda sana na kila muda niliwafikiria wao.
“pipiiiiii,,,,,pipiii” ilikuwa ni honi ya gari iliyokuwa ikiashiria kuwa kuna gari nje lililotaka kuingia ndani,,nilichungulia nje nikaona Juma ambaye ndiye milinzi mpya wa geti akiende kufungua geti ilikuruhusu gari kuingia, nilibaki palepale dirishani kutazama ni nani aliyekuwa akiingia na ndipo nilipogundua kuwa alikuwa mzee Rorbahcho,,nilipomuona nilikumbuka siku ya kwanza mzee Rorbahcho alipokuja kikazi nchini finland na kunichukua mpaka Uingereza, mzee huyu alikuwa kama baba yangu kwakuwa kila nilipomuona alikuwa akinikumbusha juu ya baba yangu,,alikuwa rafiki mkubwa sana wa kibiashara wa baba yangu hivyo mara nyingi nilimsikiliza kwa yale aliyoniambia,,siku hiyo tulipoenda Uingereza alinielezea juu ya kundi la freemasons,,ni yeye ndiye aliyenishawishi kuingia kwenye kundi hilo na baada ya kunikutanisha na mzee Richardson White mkuu wa kundi hilo nchini Uingereza basi nilikubali kwa moyo mmoja kujiunga na kundi hilo,,niliandikishwa kama mwanachama wa kundi hilo nikiwa ndani ya SURREY PROVINCIAL GRAND LODGE iliyopo kusini magharibi mwa Uingereza inayojumuisha maeneo ya Hampshire na Berkshire na mengine,,yeye ndiye aliyenitolea kiingilio na kuhakikishwa nawekwa kwenye Masoni lodge itakayoniwezesha kufanikisha kuhudhuria kila mkutano utakaofanyika,,Surrey Lodge ilikuwa inawanachama zaidi ya mia 300 na Uingereza yote katika Lodge zote zaidi ya 8000 ilikuwa inawanachama 300,000,,hivyo kuingia kwangu ndani ya kundi la freemasons kulitengeneza upya sehemu ya maisha yangu na uamini wangu,,nilidhani ningeiacha dini yangu lakini haikuwa hivyo bali niliingia katika jumuiya kubwa iliyokuwa na msaada kwangu;
*****
Nilitoka nje baada ya kuhakikisha kuwa mzee Rorbahcho alikuwa ndani ya geti langu na kwa haraka nilimfata pale alipokuwa na kusalimu na yeye aliitika,,nilimkaribisha ndani lakini hakuingia badala yake alinipa taarifa ambayo ilinifanya nilie na nianze kujuta tena;
“the angels of the light requires you to give your sacrifice today night before 00:00”(malaika wa nuru wanataka utoe sadaka yak oleo usiku kabla ya saa 6:00) aliniambia kwa sauti kavu isiyokuwa na mtikisiko wala mawimbi.
“and what’s that sacrifice”(na ni sadaka gani) nilimuuliza huku nikitetemeka,,nilitamani anijibu kuwa ilikuwa kiasi chochote cha pesa lakini si anambie ilikuwa ni mtu tena.
“you choose between Jamshid or Magret”(utachagua kati ya Jamshid au Magret),,
 
Daaaaah...isikose kusoma sehem zinazo fuata 
kwa maon tuma sms tu 
0718 363624

No comments:

Post a Comment