Thursday, December 19, 2013

Picha 22 za kijiji cha Qunu wakati wa maziko ya Mandela

 Daraja la waendao kwa miguu likipita juu ya barabara mpya ya lami inayojengwa kuelekea kijijini Qunu.
Qunu ni kijiji kidogo katika jimbo la Eastern Cape la Afrika Kusini, kilomita 32 Kusini-Magharibi ya mji wa Mthatha, katika barabara ya Butterworth na Mthata. 

Kijiji cha Mvezo, pembezoni mwa mto Mbashe, ni jirani ya mahali ambapo Mzee Nelson Mandela alizaliwa. Hapo Qunu ndipo alipokulia na aliweka nadhiri ya kurejea. 

Kijiji cha Qunu ndipo baba yake Mandela alipohamia baada ya kuvuliwa Uchifu wa Mvezo. Katika kitabu chake cha ‘Long Walk to Freedom’ Mzee Mandela amekitaja kijiji hicho kuwa ndipo alipoishi maisha ya furaha wakati wa utotoni. 

Jumapili ya Desemba 15, 2013 Mzee Mandela alizikwa kijijini Qunu katika mazishi ya Kitaifa yaliyoshuhudiwa dunia nzima. Alizikwa kwa heshima zote za kiongozi wa Taifa katika sehemu aliyochagua mwenyewe kuwa nyumba yake ya milele.

Siku ya mazishi barabara ya kuelekea Qunu ilifungwa na ni magari yaliyokuwa na kibali tu ndiyo yaliyoruhusiwa kupita


Ulinzi ulikuwa mkali kila sehemu kijijini Qunu


Wageni wakiwa katika geti kuu la nyumba ya Mzee Mandela hapo Qunu


Nyumba ya Mzee Mandela


Nyumbani kwa Madiba kijijini Qunu


Hema maalumu zilikofanyika shuguli zote za mazishi. Kaburi lake liko nje ya hema upande wa kushoto.

BOFYA READ MORE HAPO CHINI KUSHOTO KUONA PICHA ZAIDI


Hali ilivyokuwa saa kumi na moja alfajiri siku ya Jumapili


Nyumbani kwa Madiba kumejaa magari hata kabla ya jua kupanda angani


Sehemu ya kijiji cha Qunu. Mahema mbele ya nyumba ni ya wanahabari wa kimataifa waliopiga kambi hapo


Mandhari ya Qunu


Mandhari ya Qunu


Ni kijiji chenye mandhari nzuri. Wakati wa majira ya baridi barafu huanguka hapa


Qunu


Kila engo Qunu inapendeza


Kijiji cha Qunu


Bango linalotangaza kijiji cha Qunu kuwa cha urithi


Ulinzi ulikuwa si wa kawaida siku ya mazishi


Foleni ilikuwa ya kufa mtu


Wana Afrika Kusini toka kila kona walitembea umbali mrefu kwa miguu kuhudhuria mazishi


Nyimbo na ngoma vilitawala


Mdau aklipoza koo baada ya kutembea kwa muda mrefu


Sehemu ya mji wa Mthatha, kilomita kama 32 kutoka Qunu


Magari yalizuiwa kwa muda wakati mwili wa Mzee Madiba uliopowasili uwanja wa Mthatha na kupelekwa Qunu


Sehemu ya foleni ya magari ikikaribia mji wa Mthatha na hapa wakisubiri msafara wa mwili wa Mzee Mandela upite

Chanzo: othmanmichuzi.blogspot.com

No comments:

Post a Comment